Bodi ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu
(HESLB) imetuliza hasira za wanafunzi wa vyuo
vikuu kwa kurejesha posho ya chakula na malazi
ya Sh8,500 kwa kila mmoja na kwamba tofauti
baina yao itakuwa viwango vya ada.
Ufafanuzi huu uliotolewa jana usiku na Waziri wa
Elimu, Sayansi , Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi
Profesa Joyce Ndalichako wakati akizungumza
katika mahojiano maalimu na kituo cha runinga
cha Taifa -TBC utakuwa faraja kwa wanafunzi
ambao chini ya Serikali ya Wanafunzi wa Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam (Daruso) walipanga
kushinikiza walipwe posho ya Sh8,500 kwa siku
kama ilivyokuwa awali.
Hatua ya wanafunzi kujenga umoja ili kushinikiza
haki katika posho ilitokana na baadhi yao
kuingiziwa kati ya Sh40,000 na 70,000 badala ya
Sh 510,000, hali ambayo ilizua sintofahamu.
Ndalichako alisema tofauti ya malipo itakuwa
katika ada na siyo posho, “Vigezo vya mikopo
vimebadilika, kila mwanafunzi atapata fedha tofauti
lakini tumefanya marekebisho kwenye posho ya
chakula ambayo kila mwanafunzi atalipwa Sh8,500
kama awali.”
Kwa mujibu wa utaratibu wa Bodi hiyo, malipo
hayo ya chakula na malazi hutolewa kila baada ya
miezi miwili.
Mapema jana, Daruso iliwataka wanafunzi wa chuo
hicho kutotia saini fomu za fedha za mikopo yao
mpaka itakapowapa ruhusa ya kufanya hivyo.
Rais wa Daruso, Erasmi Leon alisema hayo jana
wakati akizungumza na wanafunzi wenzake kuhusu
kusudio la kwenda HESLB kwa ajili ya kutafuta
haki yao ya msingi.
“Ninachowasihi tuwe pamoja. Tuwe wamoja na
twende pamoja. Tutakwenda wawakilishi kutafuta
nafasi kwa amani waweze kusikia tuna hoja gani
lakini tukinyimwa hii nafasi tutaenda kuitafuta
tukiwa wengi,” alisema na kuongeza:
“Tuwe watulivu kwa sasa tutakapowahitaji muda
na wakati wowote kwa lolote tushirikiane ili twende
pamoja tumalize pamoja tuhakikishe tunapata
Sh8,500 kwa kila mwanafunzi kwa chakula na
malazi,” alisema.
Kuhusu suala hilo, uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar
es Salaam (UDSM) ulisema wajibu wake ni
kupokea na kusambaza majina na taarifa kutoka
Bodi kwa wanafunzi.
Akitoa ufafanuzi kwa wanafunzi waliofika ofisini
kwake kujua hatima yao na waliopata mikopo
kuchukua fomu za kutia saini, Ofisa Mikopo wa
UDSM, Lugano Mwakyusa alisema wenye jukumu
la kujua walio na sifa ya kupata mikopo ni Bodi ya
Mikopo.
“Tunaendelea kupokea majina kutoka bodi. Tayari
hapa kuna majina 949 yameshatoka, wengine tuzidi
kusubiri na wale mwaka wa pili na tatu ambao
walikuwa na mitihani ya marudio taarifa zao
zitapelekwa bodi,” Mwakyusa aliwaambia
wanafunzi waliokuwa wamejaa ofisini kwake.
Kulikuwa na hali ya sintofahamu chuoni hapo jana
baada ya wanafunzi wengi wa mwaka wa kwanza
kuonekana wakiwa wameshika bahasha za kaki
zilizokuwa na fomu za usajili wanazotakiwa kujaza
huku wakihangaika kutokana na kutojua kiasi cha
mkopo.
Juzi, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, AbdulRazaq
Badru alieleza kwamba ingawa wanafunzi 88,000
waliomba mikopo kutoka HESLB, uwezo wa bodi
hiyo ni kutoa kwa wanafunzi 21,500 pekee sawa
na asilimia 24 na waliokuwa wameshapatiwa
walikuwa 11,000 sawa na asilimia 12.
Takwimu hizi zinaonyesha zaidi ya robo tatu ya
wanafunzi wanaohitaji mikopo watakosa kutokana
na uwezo mdogo wa kifedha.
Welcome to our blog,this blog is deals with the all news about education and it allow teachers and other education dealers to discuss different things.
Thursday, 20 October 2016
MIKOPO KWA WANAOSOMA VYUO VIKUU BADO NI KIZUNGUMKUTI.
TSNP WAJIPANGA KUMFUATA WAZIRI WA ELIMU
Mtandao wa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Tanzania
( TSNP) umepanga kuunda kamati ya viongozi wa
serikali za vyuo vikuu ili kukutana kwa dharura na
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk. Joyce
Ndalichako.
Pia imepanga kuandaa tamko la kupinga tamko la
mabadiliko ya vigezo vitakavyozingatiwa katika
utoaji mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu,
lililotolewa hivi karibuni na Naibu Waziri wa Elimu
Mhandisi Stella Manyanya.
Mtandao huo umedai kuwa, mabadiliko hayo ya
vigezo yamesababisha wanafunzi wengi kukosa
mikopo huku baadhi yao kupunguziwa fedha za
kujikimu.
Mkurugenzi wa Haki za Wanafunzi TSNP, Venancy
Shitindi jana alisema kuwa TSNP kwa sasa
inakusanya taarifa za changamoto zinazo wakabili
wanafunzi waliokosa mikopo ili kuandaa tamko la
kupinga mabadiliko hayo, litakalo pelekwa katika
Ofisi ya Rais, Waziri Mkuu na Wizara ya Elimu.
“Tumepanga kutengeneza kamati ndogo ya viongozi
kwa ajili ya kukutana kwa dharura na waziri mwenye
dhamana ya elimu ili kutoa malalamiko ya wanafunzi
juu ya vigezo vipya vilivyotolewa na wizara yake, pia
tunakusanya taarifa na kuandaa tamko
tutakalolisambaza katika ofisi ya rais, wizara ya
elimu na ofisi ya waziri mkuu,” alisema.
Alidai kuwa, mtandao huo umefanya utafiti wa
vigezo vipya vilivyotajwa na kubaini kuwa
haviendani na sera ya elimu ya mwaka 2014, wala
ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) pamoja na
mpango mkakati wa kitaifa wa maendeleo kama
alivyosema Mhandisi Manyanya katika taarifa yake
aliyoitoa kwa vyombo vya habari.
“Baada ya kusoma taarifa ya Naibu Waziri Manyanya
tulikwenda kuangalia sera ya elimu ya mwaka 2014,
tukakuta hakuna sehemu iliyoainisha kundi
linalostahili kupata mkopo bali imeeleza elimu
itolewe bure na mikopo itolewe kwa kila
mwanafunzi. Na kwamba elimu imepewa kipaumbele
cha kuleta maendeleo katika nyanja zote haijasema
kwa wanaosomea masomo ya sayansi pekee,”
alisema na kuongeza.
“Hata mpango wa maendeleo wa miaka 5 yaani
2025, unaeleza kuwa Tanzania inatakiwa kuwa na
uchumi wa kati na kwamba imetoa kipaumbele elimu
kutolewa bure kwa nyanja zote ili wapatikane
wataalamu wa fani mbalimbali na wa kutosha.”
Hata hivyo, taarifa iliyotolewa na Mhandisi
Manyanya ilisema kuwa serikali kupitia Bodi ya
Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, huandaa sifa
na vigezo vya utoaji Mikopo kila mwaka ili
kuendana na malengo na matarajio yaliyopo katika
mipango na mikakati ya kitaifa kama ilivyoainishwa
katika Dira ya Taifa 2025.
Na kwamba Serikali imetoa vipaumbele katika utoaji
mikopo kwa wanafunzi wa mafunzo ya Fani za
Sayansi za Tiba na Afya,Ualimu wa Sayansi na
Hisabati, Uhandisi wa Viwanda, Kilimo, Mifugo,
Mafuta na Gesi Asilia, Sayansi Asilia na Mabadiliko
ya Tabianchi, Sayansi za Ardhi, Usanifu Majengo na
Miundombinu.
ⓒMswahili
Wednesday, 12 October 2016
SAKATA LA MBEYA DAY RC KAYAONGEA HAYA
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makala
amesema kuwa wanafunzi wa ualimu na walimu
waliohusika na tukio la kumpiga mwanafunzi
katika Shule ya Sekondari ya Kutwa Mbeya tayari
wanaendelea kuhojiwa na Jeshi la Polisi kufuatia
tukio hilo.
Licha ya kuwa tukio lile halikuwa adhabu sahihi
kwa mwanafunzi, Mkuu wa Mkoa amewataka
wazazi kujijengea tabia ya kuwafuatilia watoto wao
kwani ameleeza kuwa nidhamu ya wanafunzi wa
shule hiyo ni mbovu sana hasa kwa wanafunzi wa
kidato cha tatu na cha nne.
Mkuu wa mkoa ameeleza kuwa, kuna wakati
darasa lenye wanafunzi 50, mwalimu anafundisha
wanafunzi 10 pekee wengine wakiwa hawamo
darasani na mara kadhaa wanapishana na
mwalimu wakati wanaingia wao wanatoka.
Wanafunzi wengine wamediriki hata kukunjiana
ngumi na walimu, hivyo baadhi ya walimu ili
kuepusha shari wamewaacha wafanye waoonavyo
vyema.
Mkuu wa mkoa amesema kuwa wataendelea
kufanya uchunguzi kuwabaini wanafunzi wakarofi
zaidi na adhabu stakihi zitachukua hatua mara
moja ili kuweza kurejesha nidhamu katika shule
mkoani humo.
***********************************
Mswahili
Sunday, 9 October 2016
EWE MTUMISHI JIANDAE KWA HILI
Hatua ya Baraza la Mitihani nchini (Necta) kutoa
ratiba ya kufanya uhakiki wa vyeti vya kidato cha
nne, sita na ualimu kwa watumishi wote wa umma
sasa ni wazi imezidi kupandisha joto kwa vigogo na
watumishi mbalimbali ambao hawana sifa za kielimu
kushika nafasi walizo nazo.
Katika taarifa yake ya sasa Baraza la Mitihani
nchini, limetangaza kuwafuata katika maeneo yao
ya kazi watumishi wote walioko katika mamlaka za
mikoa, halmashauri na manispaa kwa ajili ya
kufanya uhakiki wa vyeti vyao hivyo vya kitaaluma.
Kwa mujibu wa barua iliyosainiwa na Edga Kasuga
kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa Baraza hilo
kwenda kwa Makatibu tawala wa Mikoa, uhakiki
utafanyika katika ofisi za Makatibu Tawala wa
mikoa kuanzia Oktoba 10 hadi 14 mwaka huu,
ingawa ratiba nyingine ya uhakiki imeonyesha zoezi
hilo litafikia tamati Novemba 7 mwaka huu.
“Ili kufanikisha zoezi hilo Baraza limetaka kupata
orodha (nakala- laini ya soft copy) ya watumishi
wote wa umma waliopo katika Mkoa, Halmashauri
na Manispaa.
“Nakala za vyeti vya kidato cha nne, cha sita na
ualimu vya watumishi wote walioandikishwa na
chumba cha kufanyia uhakiki,” inaeleza taarifa
hiyo ya Baraza la Mitihani.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Baraza la
Mitihani, uhakiki huo utafanywa katika makundi
matano katika mikoa tofauti tofauti.
Oktoba 10, mwaka huu kundi la kwanza litafanya
uhakiki katika Mkoa wa Mtwara, kundi la pili
Singida, kundi la tatu Rukwa, kundi la nne Katavi
na kundi la tano litakuwa Geita.
Oktoba 17 mwaka huu, kundi la kwanza litakuwa
Lindi, la pili Manyara la tatu Songwe, la nne
Kigoma na la tano litakuwa Mwanza.
Oktoba 24 mwaka huu, kundi la kwanza litakuwa
Morogoro, la pili Arusha, la tatu Mbeya, la nne
Tabora na la tano Mara.
Oktoba 31 mwaka huu, kundi la kwanza litakuwa
Pwani, la pili Kilimanjaro, tatu Ruvuma, la nne
Shinyanga na la tano Simiyu.
Novemba 7 mwaka huu, kundi la kwanza litakuwa
Dar es Salaam, la pili Tanga, la tatu Njombe, la
nne Dodoma na la tano Iringa.
FAGIA FAGIA WIZARA YA ELIMU YAENDELEA
Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya
Ufundi imezifuta shule nyingine za awali na msingi
nchini ambazo hazijasajiliwa zaidi ya 10 kuanzia
Desemba mwaka jana. Aidha, shule tano kati ya 40
zilizokuwa zimefutiwa usajili zimekamilisha taratibu
na kurejeshewa usajili wake.
Kaimu Mkurugenzi wa Usajili wa Shule katika
wizara hiyo, Khadija Mcheka amesema mpaka sasa
bado wanaendelea na ukaguzi kubaini shule ambazo
hazijasajiliwa.
Alizitaja shule ambazo zimefutwa kwa kutosajiliwa
kuwa ni Mwandai Junior Academy, shule ya msingi
DACETE, shule za msingi Malaika na Fares Kisingo
(FK) za wilaya ya Kinondoni. Nyingine ni shule ya
msingi The Unity, shule ya sekondari Jotac iliyopo
eneo la Kipunguni, Verena iliyopo eneo la Pugu
zote wilaya ya Ilala, Exodus iliyopo Kigamboni na
Havard Junior ya wilaya ya Temeke.
Alisema shule nyingine zilizofutwa kabisa ni shule
ya sekondari ya Kahe ambayo imefutwa kutokana
na wamiliki kushindwa kuiendesha na pia majengo
yake yamebadilishiwa matumizi.
Alisema shule nyingine za Deogrolius International
School iliyopo Kitunda, Desinity na Almustakim
zote za jijini Dar es Salaam nazo zimefutiwa
usajili. Alisema awali yalitolewa majina ya wamiliki.
Mcheka alisema pia shule mbili hazitakiwi kuwa za
bweni ambazo ni Heritage iliyopo Banana Ukonga
na Hellens iliyopo Kinondoni.
Akizungumzia shule zilizorejeshewa usajili, alisema
ni Gisera, Rose Land, Conerstone na Grace za
jijini Dar es Salaam na Must Lead na Qunu zilizopo
mkoani Pwani huku shule ya Fountain Gate
ikifutiwa usajili wa kuendesha shughuli za bweni.
Akifafanua kuhusu shule ya Coner Stone alisema
baada ya ukaguzi na kufutiwa usajili kuanzia mwezi
Julai zipo shule ambazo zilikamilisha utaratibu na
kurejeshewa usajili, na kwamba hakuna shule
iliyoelezwa kufutiwa usajili kwa uongo.
“Kuhusu shule zinazolalamika kutangazwa kimakosa
si kweli isipokuwa jambo lililofanyika baada ya
kuwapelekea barua kuwataka kutawanya wanafunzi
baada ya kufutiwa usajili walikamilisha utaratibu
ndipo wakasajiliwa,“ alisisitiza.
Alisema ukaguzi huo wa shule unaendelea katika
mikoa yote nchini kwa kuwatumia wakaguzi wa
Kanda na watakaobainika watafutwa mpaka
watakapokidhi vigezo vinavyotakiwa.
Hivi karibuni Mcheka alisema kuanzia Julai hadi
Desemba mwaka jana, waligundua kuwepo kwa
shule 35 zisizosajiliwa na kuzifuta na baadaye
walizifungia shule nyingine 12.
Mcheka alisema shule zinaweza kufutwa kwa
sababu mbili zikiwamo zilizosajiliwa, lakini zikakiuka
vigezo ambapo zikitimiza vigezo zinaweza kuomba
upya usajili na kupewa.
“Lakini aina ya pili ni zile ambazo hazijasajiliwa na
zinaendeshwa kinyume cha sheria ambazo nazo
zikifuata taratibu zikatimiza vigezo zinaweza
kupewa usajili,” alifafanua Kaimu Mkurugenzi huyo
wa Usajili wa Shule.
Alisema katika kipindi hicho mpaka Agosti mwaka
huu baada ya tangazo la kuwataka kusajiliwa shule
za awali nne, zile za awali na msingi 105 na
sekondari 19, walifika wizarani kwa ajili ya kupata
taratibu za usajili ambapo zipo zilizosajiliwa na
nyingine kupewa vibali.
Alisema katika usajili, wapo waliokidhi viwango na
wengine walipatiwa maelekezo na kupatiwa vibali
vya kutumia majengo yaliyopo huku wengine
wakipewa vibali vya kujenga majengo ya shule
kabla ya kupata usajili.
Alisema kwa shule walizozifungia, waliwaandikia
barua za kuwafungia na kuwataka kuhakikisha
wanawatawanya wanafunzi katika shule
zilizosajiliwa kwa gharama zao bila kuwaathiri
wanafunzi.
Alitaja shule zilizofungiwa kwa kuendesha shughuli
zake bila usajili kuwa ni shule ya awali na msingi
Must Lead ya mkoa wa Pwani, kwa upande wa
mkoa wa Dar es Salaam ni Brainstorm, Pax,
Lassana, Grace, Rose Land, Julius Raymod, St
Thomas, Mary Mother of Mercy, Noble Sinkonde,
Immaculate Heart of Mary, St Columba, Corner
Stone, Dancraig, Mwalimu Edward Kalunga, Edson
Mwidunda, Gisela, Kingstar, St Columba, Bilal
Muslim, Thado, Hocet , Elishadai, Lawrance
Citizen, Comrade, Dar Elite Preparatory, Golden
Hill Academy na Hekima.
Nyingine ni Pwani Islamic, St Kizito na Rwazi
Encysloped za Kagera, Dancraig na Qunu za Pwani,
Hellen’s ya Njombe, Joseph ya Arusha, Samandito
na Maguzu za Geita. Alizitaja shule za sekondari
zilizofungiwa kwa sababu hiyo kuwa ni Hananasif,
Elu, Hocet, Safina za Dar es Salaam na Namnyaki
ya Iringa.
Tuesday, 13 September 2016
CWT:MADENI YA WALIMU HAYAJAKWISHA
Hayo yamesemwa na rais wa chama cha walimu Tanzania Bw. Gracian Mukoba kufuatia kauli iliyotolewa na serikali mwishoni mwa wiki iliyopita kupitia waziri wa mwenye dhamana Prof. Joyce Ndalichako kuwa serikaili tayari imekamiliza kulipa madeni yote ya walimu. Akizungumza na waandishi wa habari jana rais wa chama cha walimu amesema kuwa taarifa hizo sio sahihi kwa sababu bado kuna walimu kutoka halmashauri mbalimbali bado wanaidai serikali madeni mbalimbali yakiwemo yasiyokuwa ya mishahara,aliongeza kuwa hakufuraishwa na hatua hiyo ya serikali kutoa taarifa hizo kwani zinaweza kuwafanya walimu wafikiri kuwa serikali inataka kuwadhulumu pia ameitaka serikali kupitia tena madeni ya walimu ili kuondoa sintofahamu ambayo inaweza kujitokeza katika siku zijazo.
WANAFUNZI WAWATANDIKA FIMBO WALIMU WAO
Wawanafunzi wa Kidato cha Sita Shule ya
Sekondari Usevya wilayani Mlele Mkoa wa Katavi,
wanadaiwa kuwashambulia kwa kuwacharaza viboko
walimu wao wawili miongoni mwao akiwemo Makamu
Mkuu wa Shule hiyo, Makonda Ng’oka
“Membele'‘ (34) ambaye ameng’olewa meno
matano kwa kipigo hicho.
Walimu hao wawili wamedai kuwa hawako tayari
kuendelea kufundisha katika shule hiyo huku
wakisisitiza kuwa ni fedheha kwao kucharazwa
viboko na wanafunzi wao wenyewe ambapo Mwalimu
Gabriel Kambona aliachwa na ngeu kichwani.
Mei mwaka huu, Ng’oka “Membele” alifikishwa
katika Mahakama ya Mkoa wa Katavi kwa tuhuma
za kumlawiti mwanafunzi wake akidaiwa kutenda
kosa hilo kati ya Novemba 2015 na Aprili mwaka
huu.
Ilisemekana kukamatwa na kufikishwa mahakamani
kwa Makamu Mkuu huyo wa shule hiyo kulifuatia
wanafunzi wa kiume wanaosoma Kidato cha Tano
sasa wako Kidato cha Sita katika shule hiyo
kumkataa na kutishia kuandamana kupinga vitendo
vyake vya kuwalawiti wanafunzi wake.
Wanafunzi hao walidai kuwa mwalimu huyo
amekuwa akiwalawiti baadhi yao ikiwa ni adhabu
mbadala wanapobainika kufanya makosa shuleni
hapo.
Hata hivyo, baada ya kutopatikana ushahidi wa
kumtia hatiani Ng’oka, Julai 27, mwaka huu
Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Wilaya ya Mpanda
ilimwachia huru.
Mwalimu Ng’oka aliripoti kwenye kituo chake cha
kazi shuleni Usevya Agosti Mosi mwaka huu ambako
kurejea kwake shuleni hapo kunadaiwa kuamsha
hasira kwa baadhi ya wanafunzi wa Kidato cha Sita
wakidai hawapo tayari kumwona mwalimu huyo na
familia yake shuleni hapo.
Akizungumza na wanahabari jana mjini hapa,
Ng’oka alidai kuwa hayuko tayari kuendelea
kufundisha kwenye shule hiyo akihofia usalama
wake na kutokana na kipigo alichokipata cha
kushambuliwa na baadhi ya wanafunzi wake wa
kidato cha tano na cha sita wakati akiwa nyumbani
kwake na familia yake.
Akisimulia mkasa huo, alisema Agosti 12, mwaka
huu usiku alikuwa nyumbani kwake shuleni hapo
pamoja na familia yake pamoja na mwalimu
mwenzake, Gabriel Kambona aliyekuwa
amemtembelea.
“Ghafla, saa mbili usiku nikiwa maliwatoni nikioga
lilitokea kundi la wanafunzi wa kidato cha tano na
sita wakiwa na silaha za jadi kama vile fimbo,
marungu, mawe na matofali na kuanza
kuishambulia familia yangu pamoja na mwalimu
Kambona,” alieleza na kuongeza kuwa alilazimika
‘kuchomoka’ bafuni baada ya kusikia mayowe
yaliyokuwa yakipigwa na familia yake wakiomba
msaada. Alipofika sebuleni alishuhudia wanafunzi
hao wakiishambulia familia yake kwa kuwacharaza
viboko.
“Ndipo walinigeukia na kuanza kunishambulia kwa
kunipiga kwa marungu na fimbo hadi nikapoteza
fahamu nilizinduka nikiwa nimelazwa kwenye Kituo
cha Afya Usevya na kubaini kuwa nimepoteza meno
yangu matano huku nikiwa nimejeruhiwa vibaya
kichwani. Baadaye nilihamishiwa katika Hospitali
ya Wilaya ya Mpanda ambako nililazwa wiki moja na
nusu kwa matibabu na sasa nimepewa rufaa niende
Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar kwa
matibabu zaidi,” alieleza.
Alidai kuwa uhasama baina yake na wanafunzi hao
umedumu kwa muda mrefu, lakini anashangaa
uongozi wa Halmashauri ya Mpimbwe na Wilaya ya
Mlele umeshindwa kumpangia kituo kingine cha
kazi na kuchukua hatua yoyote kwa wanafunzi hao
licha ya kupeleka majina yao kwa kuwa
anawafahamu wote waliohusika.
Mwalimu Kambona alidai kuwa hayuko tayari
kuendelea kufundisha kwenye shule hiyo kwamba
kitendo cha kupigwa na wanafunzi wake
kimemfedhehesha.
Kwa mujibu wa mwalimu huyo, walimu wa shule hiyo
waliketi baada ya kutokea kwa tukio hilo, na
walifikia maamuzi kuwa wanafunzi wote
waliobainika kushiriki kuwashambulia walimu wao
wasimamishwe shule akidai kuwa uongozi wa
Halmashauri ya Mpimbwe na Wilaya ya Mlele
ulipinga.
“Nimeandika barua ya kuomba uhamisho kwani nia
aibu kwangu kuendelea kufundisha wanafunzi
ambao wamenishambulia na kunitoa ngeo kichwani
….. siku hiyo ya tukio niliibiwa simu mbili za
kiganjani lakini jana nimefanikiwa kuikamata simu
moja kwa mwanafunzi wa kidato cha tano
anayeitwa , Alex Maiko Makona na tayari
amemfikisha katika Kituo cha Polisi cha Usevya,”
alidai.
Mwenyekiti wa Chama cha Walimu (CWT) Mkoa wa
Katavi, Gregori Mshota alisema tayari chama
chake kimeanza kuwasiliana na uongozi wa
Halmashauri ya Mpimbwe na uongozi wa Wilaya ya
Mlele ili kuhakikisha mwalimu huyo anakuwa
salama.
Ofisa Elimu wa Mkoa wa Katavi, Ernest Hinju
alidai kuwa suala hilo lipo ofisini kwake na
wameanza kulitafutia ufumbuzi. “Jambo hili
linahitaji ushirikishwaji wa vyombo mbalimbali
ikiwemo Bodi ya Shule ya Sekondari ya Usevya,”
alieleza.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipokuwa katika
ziara mkoani Katavi mwezi uliopita, mke wa
mwalimu Ng’oka alitinga kwenye mkutano wa
hadhara uliofanyika kijijini Maji Moto akiwa na
bango lenye malalamiko ya kutishiwa usalama wa
maisha wa familia yake, na Waziri Mkuu alimwagiza
Kamanda wa Polisi wa Mkoa kushughulikia
malalamiko hayo.
CHAGUZI KWA WALIOOMBA VYUO VIKUU
Tume ya vyuo vikuu imetoa orodha ya majina ya waliochaguliwa katika vyuo mbalimbali nchini kuangalia bofya hapa👇 http://cas.tcu.go.tz/cas_core/index
AJIRA MPYA ZANUKIA
Serikali imeanza kupanga walimu wa sayansi moja
kwa moja katika shule badala ya Halmashauri kama
ilivyokuwa awali ili kuleta uwiano sawa wa walimu
katika shule mbalimbali nchini.
Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Rais (TAMISEMI) Suleman Jaffo alipokuwa
akijibu swali la Mbunge wa Muleba Prof. Anna
Tibaijuka lililohusu mkakati wa Serikali katika
kukabiliana na tatizo la upungufu wa walimu.
Naibu Waziri Jaffo amesema kuwa Serikali
imeandaa mkakati wa kuwaajiri wahitimu wa
shahada za sayansi ambazo siyo za ualimu baada ya
kuwapa mafunzo ya muda mfupi kuhusu mbinu za
ufundishaji na maadili ya ualimu ili kukabiliana na
changamoto ya walimu wa sayansi nchini.
Naibu Waziri Jaffo amesema kuwa tayari kibali
kimeombwa katika Ofisi ya Rais Utumishi kwa ajili
ya utekelezaji huo, ambapo Serikali imepanga
kuajiri walimu wastaafu wenye uwezo wa
kufundisha waliokuwa wanafundisha masomo ya
sayansi kwa mkataba ili kupunguza pengo lililopo.
Aidha, Naibu Waziri Jaffo amebainisha kuwa
Serikali inafanya tathimini ya mahitaji ya walimu
wa masomo ya sanaa kwa kila Halmashauri ili
kubaini maeneo yenye ziada na yenye upungufu ili
kusawazisha.
“Mpango wa Serikali uliopo ni kuwahamasisha
walimu wa ziada wa masomo ya sanaa kwenda
kufundisha katika shule za msingi ndani ya
Halmashauri husika, ambapo kabla ya kuanza
utekelezaji wa mabadiliko haya Serikali itatoa
waraka maalumu kwenda katika Halmashauri zote
nchini ” amefafanua Naibu Waziri huyo.
Akizungumzia kuhusu utaratibu wa mafunzo ya
walimu Mhe. Jaffo amesema kuwa Halmashauri
moja haiwezi kuwa na mfumo wa peke yake wa
kuandaa walimu hali ambayo iltakuwa ni vigumu
kuthibiti ubora wa mafunzo hayo kwa walimu.
Hata hivyo amesema kuwa Serikali itaendelea
kuongeza udahili wa walimu wa sayansi katika vyuo
vya ualimu kadri watakavyojitokeza ili kukidhi
mahitaji yaliyopo
Saturday, 10 September 2016
WAZIRI:TUMESHAMALIZANA NA WALIMU
WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia
na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce
Ndalichako amesema hadi sasa wizara
hiyo haina deni inayodaiwa na walimu
nchini na kwamba madeni yaliyokuwepo
ya Sh bilioni 22 yalishalipwa.
Profesa Ndalichako alisema hayo juzi
jioni wakati akizungumza kwenye
kipindi cha Tunatekeleza
kinachorushwa hewani moja kwa moja
na Kituo cha Televisheni cha Shirika
la Utangazaji Tanzania (TBC1).
Akizungumzia madeni ya walimu,
alisema serikali inawajali walimu
nchini na zipo jitihada mbalimbali
zimekuwa zikifanywa kuhakikisha madai
yao yanahakikiwa na kulipwa ili
kuepuka malimbikizo.
Alisema madeni ya walimu yako ya
aina mbili; moja ni madeni ya
mishahara ambayo wao wizara
hawayashughulikii bali yapo chini ya
Ofisi ya Rais, Utumishi na kwamba
madai aina ya pili ni yale yasiyo na
mshahara kama vile likizo, matibabu
na mengineyo, ambayo yako chini ya
wizara yake na hadi sasa wameshalipa
Sh bilioni 22 na hakuna madeni
mengine kutoka kwa walimu na
kuwataka walimu nchini kama wana
madeni mapya kuanzia sasa
wayawasilishe wizarani kwa ajili ya
kuhakikiwa na kulipwa.
“Wizara tunatambua mchango wa walimu
na umuhimu wao kwa upande wetu,
hatuna madai yoyote ya walimu yale
yanayotuhusu, kwa sababu huwa tuna
utaratibu wa kulipa kadri
tunavyoyapata na kama yapo kwa sasa
wayalete, fedha za kulipa zipo,”
alisema Profesa Ndalichako.
Akizungumzia suala la watumishi
hewa, Profesa Ndalichako alisema ni
vyema walioguswa katika uhakiki huo
unaoendelea kufanywa na timu ya
watendaji kutoka taasisi mbalimbali,
wakiwemo wakurugenzi, wakajiondoa
wenyewe kwenye ajira kwa sababu
mashtaka yanawangoja.
Kuhusu uhakiki wa wanafunzi wa elimu
ya juu, Profesa Ndalichako alisema
hadi sasa wamekamilisha uhakiki wa
vyuo 31 kati ya vyuo 80 vilivyopo
nchini na wameshabaini wanafunzi hewa
2,921 ambao hawakujitokeza wakati wa
uhakiki, licha ya matangazo na
msisitizo kutolewa.
Profesa Ndalichako alisema wakati
kazi ya uhakiki ilipoanza, walitoa
matangazo katika vyuo vyote na pia
vyuo navyo vilitoa matangazo kwenye
mbao za matangazo vyuoni na pia
kupitia vyombo vya habari na pia
kupitia serikali ya wanafunzi katika
vyuo husika, lakini idadi hiyo
haikujitokeza kuhakikiwa.
Alisema kwa wale wachache waliopuuza
kuhakikiwa hata kama wako mwaka wa
mwisho wa masomo, bado watatambulika
kama wanafunzi hewa hadi pale
watakapohakikiwa na hiyo itawagharimu
kulipa gharama za kufanyiwa uhakiki
huo.
Akizungumzia changamoto za wanafunzi
kutojua kusoma na kuandika, Profesa
Ndalichako alisema serikali imekuwa
imetoa mafunzo kwa walimu
wanaofundisha darasa la kwanza na la
pili na kwamba kadri muda
unavyosonga ndivyo tatizo
linavyoondoka.
Kuhusu utaratibu wa utoaji mikopo
kwa elimu ya juu, Profesa Ndalichako
alisema changamoto zipo kutokana na
mfumo uliokuwa ukitumika, lakini
hatua zimeshaanza kuchukuliwa ili
kuuboresha ili kuhifadhi kumbukumbu
za wanufaika ili iwe rahisi kuzidai.
Aidha, alisisitiza wanafunzi
waliomaliza shahada zao katika vyuo
mbalimbali nchini na ikagundulika
kuwa walizipata kwa njia ya rushwa,
ikibainika watanyang’anywa.
Chanzo: Habari Leo.
Tuesday, 6 September 2016
ONYO KWA WASIMAMIZI MTIHANI WA DARASA LA SABA
Na Almasi Mswahili
Ikiwa yamesalia masaa kadhaa kabla ya kuanza kwa mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi hapo kesho na kesho kutwa (Jumatano tarehe 7/9/2016 na Al-hamis tarehe 8/9/2016)
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya
Ileje Haji Mnasi, amewaasa wasimamizi wa mitihani
ya kumaliza elimu ya msingi kutofanya kazi kwa
mazoea ili kutoruhusu mianya itakayowafanya
wanafunzi wasiokuwa na uelewa kufaulu mitihani
hiyo.
Alisema kumekuwa na baadhi ya wanafunzi
wasiojua kusoma na kuandika wanafaulu mithani
hiyo kitendo kinachotia mashaka kwa wasimamizi
hao kushindwa kunyakazi waliyopewa kwa makini.
Mnasi aliyasema hayo jana, wakati akitoa semina
ya mafunzo kwa wasimamizi wa halmashauri ya
wilaya ya Ileje ambapo alisema usimamizi hafifu wa
mitihani umesababisha kuwepo kwa watumishi
wasiokuwa na uwezo kitaaluma.
Aidha kabla ya uteuzi wa Rais wa jamhuri ya
muungazo wa tanzania Dr John Pombe Magufuli
mkurugenzi huyo ambaye kitaaluma ni mwalimu
alikuwa afisa elimu shule ya msingi manispaa ya
iringa alisema iwapo ikibainika kufaulu kwa
wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika mtuhumiwa
wa kwanza kwenye uzembe huo atakuwa msimamizi
wa mitihani na hatua kali zitachukuliwa zidi yake.
“Nawatahadharisha kwamba mnaweza mkarubuniwa
kuwawezesha wanafunzi wasiokuwa na sifa wafaulu
mitihani hiyo,kufanya hivyo ni kukiuka kanuni za
usimamizi na uendeshaji wa mtihani na kuwaambia
hayupo tayari kutumbuliwa na rais kwasababu za
wasimamizi”alisisitiza Mnasi.
Hata hivyo Mnasi aliwataka wasimamizi hao kuwa
makini katika kufanyakazi hiyo na kama kuna
jambo lolote ambalo hawajalielewa kuhusu kazi hiyo
ni vyema wakauliza ili kupewa majibu.
“hakikisheni kuwa taratibu zote za mitihani
zinazingatiwa ipasavyo na kuwataka wasimamizi
wote kufanya kazi yao kwa umakini na uadilifu wa
hali ya juu.“Nawaasa wasimamizi wa mitihani
kujiepusha na vitendo vya udanganyifu kwani
serikali itachukua hatua kali kwa yeyote
atakayebainika kukiuka taratibu za mitihani,”
alisema Mnasi.
Mnasi alibainisha kuwa, serikali imezingatia uwezo
wa kitaaluma, uadilifu na uaminifu hivyo
wasimamizi hao kupewa jukumu la kusimamia
mitihani hiyo muhimu ya kitaifa.
Aliongeza kuwa mitihani hiyo ni muhimu ili
kuliwezesha taifa kupima kiwango cha elimu
kilichpo nchini na kuwapata wasomi wa kiwango cha
juu.
Nao wasimamizi wa mitihani hiyo wamemuahidi
mkurugenzi huyo kuwa watasimamia mitihani hiyo
kwa kufuata sheria na kanuni za usimamizi wa
mitihani walizopewa.
Saturday, 3 September 2016
WIZARA YA ELIMU YATAKIWA KUONGEZA WATAALAMU WA AFYA
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameitaka Wizara ya
Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi iweke mpango
maalumu wa kuongeza wataalamu zaidi katika
sekta ya afya ndani ya nchi ili kuipunguzia Serikali
gharama za kusomesha wataalam hao nje ya nchi.
Ametoa agizo hilo Ijumaa, Septemba 2, 2016
wakati alipokagua maendeleo ya mradi wa ujenzi
wa Kampasi ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Afya na
Sayansi ya Tiba Muhimbili (MUHAS) na Ujenzi wa
Kituo cha Tiba cha Kimataifa cha Muhimbili katika
eneo la Mloganzila.
Amesema Serikali zilizotangulia zimefanya kazi
kubwa na nchi imefikia hatua nzuri ya kuongeza
wataalam ndani ya nchi ambao watakwenda
kutatua changamoto ya upungufu wa madaktari
bingwa kwenye hospitali za mikoa na wilaya.
Waziri Mkuu amesema ujenzi wa kituo hicho cha
tiba cha kimataifa pia utawapunguzia wananchi
adha ya kutafuta fedha za kwenda kupata
matibabu nje ya nchi. Tayari upasuaji mkubwa wa
magonjwa ya moyo umeanza kufanyika nchini.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amemuagiza
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Bw. Humphrey
Polepole awasake watu wote waliohusika na wizi wa
lita 1,000 za mafuta ya kuendeshea mitambo
katika karakana ya mkandarasi anayejenga
Kampasi hiyo.
“Wafanyakazi waache wizi. Lita 1,000 zinaondokaje
katika karakana ya mkandarasi? Hii kampuni
inayolinda kama imeshindwa kazi iondolewe na
Mkuu wa wilaya usimhurumie mwizi,” amesisitiza.
Kwa upande wake Waziri wa Elimu, Sayansi na
Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako amesema
kukamilika kwa kampasi ya Mloganzila kutasaidia
upatikanaji wa madaktari bingwa wengi nchini
ambao watapunguza gharama za kupeleka
wagonjwa kwenda kutibiwa nje ya nchi.
Awali, Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Ephata
Kaaya alisema kukamilika kwa hospitali pamoja na
kampasi yote ya chuo kutawezesha kupunguza kwa
kiasi kikubwa uhaba wa wataalamu wa afya nchini.
Amesema hospitali hiyo itatumika kutoa huduma za
afya za kitaalam zaidi kwa magonjwa mbalimbali,
hivyo kupunguza idadi ya wagonjwa wanaopelekwa
nje ya nchi kwa matibabu. Pia itapunguza
msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Taifa
ya Muhimbili.
Ujenzi wa mradi huo umegharimu Dola za
Kimarekani milioni 61, ambapo Serikali imetoa Dola
milioni 18 na Serikali ya Korea imetoa mkopo wa
Dola milioni 43. Kukamilika kwa ujenzi wa kampasi
hiyo ya Mloganzila kutawezesha chuo kuongeza
idadi ya udahili wa wanafunzi wa fani ya afya
kutoka 4,010 hadi 15,000.
Prof. Kaaya amesema mkataba wa awamu ya
kwanza ya ujenzi wa mradi huo ulisainiwa tarehe
12, Desemba, 2014 na ujenzi ulianza mwezi Julai,
2015 na unatarajiwa kukamilika Oktoba, 2016.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
Friday, 2 September 2016
TCU YATANGAZA UDAHILI AWAMU YA PILI
Tunapenda kuutangazia Umma kuwa tulifunga
mfumo wa pamoja wa udahili tarehe 31/08/2016
saa sita usiku ili kuchakata maombi ya waombaji
waliofanikiwa kuomba udahili kwa mwaka wa
masomo 2016/2017.
Hata hivyo kutokana na wengine kushindwa
kufanikiwa kutokana na sababu mbali mbali, Tume
inatangaza kuwa itafungua maombi kwa awamu ya
pili kuanzia tarehe 12 hadi 23 Septemba 2016 ili
kuruhusu makundi yafuatayo kuomba udahili.
1. Waombaji watakaokuwa wamekosa nafasi
kwenye awamu ya kwanza
2. Waombaji wa kidato cha Sita walioshindwa
kuomba katika awamu ya kwanza
3. Waombaji wenye vigezo vya Stashahada ambao
walishindwa kuomba kutokana na matokeo yao
kuchelewa kufika NACTE kwa wakati,
4. Waombaji ambao wamemaliza mitihani ya
“Cambridge” mwaka 2016 na matokeo yao
yameshatoka,
5. Waombaji waliofaulu mitihani ya RPL,
6. Waliokuwa wanafunzi wa vyuo vikuu watakao
kuwa na uthibitisho toka vyuo vyao vya awali.
Baada ya hapo Tume haitaruhusu tena maombi ili
kuruhusu taratibu zingine za kiudahili kuendelea
kwa ngazi ya Bodi ya Mikopo na vyuoni.
Asanteni
Imetolewa na
Prof. Eleuther Mwageni
Kaimu Katibu Mtendaji
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania
02 Septemba 2016
Sunday, 21 August 2016
AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA 30 JELA KWA KUMBAKA MWANAFUNZI WA MIAKA 9
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi wilayani Urambo
mkoani Tabora, imemuhukumu Deus Barnaba(45)
kifungo cha miaka 30 jela baada ya kumkuta na
hatia ya kumnajisi mwanafunzi wa darasa la tatu
mwenye umri wa miaka tisa.
Akitoa hukumu hiyo mwishoni wa wiki iliyopita,
Hakimu Mkazi, Baptista Kashusha, alisema
mahakama imeridhika na ushahidi uliotolewa na
upande wa mashitaka hivyo kumuona mshitakiwa
ana hatia.
Alisema adhabu hiyo iwe fundisho kwa watu
wengine wenye nia ya kufanya vitendo hivyo.
Hakimu Kashusha alisema mashahidi nane
walioletwa mahakamani hapo walithibitisha kuwa
mshitakiwa alitenda kosa hilo.
Mashahidi hao ni pamoja na daktari aliyempokea
mlalamikaji na kutoa fomu namba tatu (PF3)
iliyoonesha kuwa binti huyo aliumizwa katika
sehemu za siri.
Awali, Mwendesha Mashitaka wa Polisi, ,Joseph
Mbwana, alieleza mahakama hiyo kuwa Machi 27,
mwaka huu, majira ya saa 2:00 usiku katika kijiji
cha Mwangaza wilayani Urambo, Deus alimnajisi
binti mwenye umri wa miaka tisa na kumsababishia
maumivu makali katika sehemu zake za siri.
Aidha, aliiomba mahakama itoe adhabu kali kwa
mshitakiwa ili kukomesha matendo ya ubakaji
kabisa kwani mtuhumuwa anaonekana ni mtu
mwenye akili timamu, alifanya hivyo kwa makusudi
tu.
Hata hivyo, mshitakiwa huyo aliiomba mahakama
impunguzie adhabu kwakuwa ni mkosaji wa mara ya
kwanza na ana wazazi, mke na watoto
wanaomtegemea.
WATUMISHI HEWA WAONGEZEKA
Taarifa rasmi ya mwisho ya utekelezaji wa zoezi la
kuwaondoa watumishi hewa serikalini na taasisi
zake zote, itawasilishwa kwa Rais John Magufuli
Ijumaa wiki ijayo.
Hadi sasa
wameshabainika watumishi hewa 16,127 na
wameondolewa kwenye mfumo wa utumishi.
Aidha, mbali ya serikali kuokoa Sh bilioni 16.15
kwa mwezi huu wa Agosti baada ya watumishi hewa
hao kuondolewa kwenye mfumo wa utumishi, ambao
kama wasingeondolewa fedha hizo zilikuwa ziwalipe
mshahara, posho na malipo mengine, waajiri 145
hawajawasilisha taarifa kuhusu uhakiki wao.
Hayo yamebainishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora,Mh. Angella Kairuki alipozungumza na
waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam
kuhusu utekelezaji wa agizo la Rais Magufuli la
kuwataka waajiri wote wa umma na serikali,
kuwaondoa watumishi hewa.
Akifafanua taarifa hiyo, Kairuki alisema Agosti
26, mwaka huu watamkabidhi rais taarifa rasmi ya
utekelezaji wa agizo hilo huku akiwataka waajiri
145 ambao hawajawasilisha taarifa za ama uwepo
wa watumishi hewa au la, kuhakikisha
wanaziwasilisha taarifa hizo kabla ya Ijumaa wiki
ijayo.
“Tunawapa muda hadi Ijumaa wiki ijayo wawe
wamewasilisha taarifa za kama wana watumishi
hewa au la na sisi Agosti 26, mwaka huu ndio
tunamkabidhi rais taarifa rasmi ya mwisho ya
utekelezaji wa agizo alilotoa,” alisema Kairuki
akizungumzia hatua ya Rais Magufuli kuagiza
uhakiki huo Machi mwaka huu.
Akielezea hatua zilizochukuliwa hadi sasa na waajiri
hao, Kairuki alisema nchi ina jumla ya waajiri 409
wa serikali na taasisi mbalimbali za umma, na kati
ya waajiri hao, hadi sasa waajiri 264 ndio
waliowasilisha taarifa za utekelezaji wa agizo hilo.
Alisema kati ya waajiri hao 264 waliowasilisha,
waajiri 63 wamethibitisha hawana watumishi hewa,
huku waajiri 201 wakibaini uwepo wa watumishi
hewa kuanzia mmoja na kuendelea.
“Tumepokea taarifa za utekelezaji wa agizo la rais
alilitoa Machi 15, mwaka huu na hadi sasa waajiri
264 kati waliotekeleza agizo hilo, 201 wamebaini
wana watumishi hewa,”
alisema Kairuki.
Akizungumzia hatua zitakazochukuliwa baada ya
kufikia tarehe ya mwisho wa kupeleka taarifa hizo,
Kairuki alisema jukumu lao ni kuzipokea na
kukabidhi mamlaka ya uteuzi ambayo ndiyo iliagiza
na ambayo ndiyo itaamua hatua za kuchukua.
Sambamba na hilo, Kairuki alisema hadi sasa jumla
ya watumishi hewa 606, wameanza kuchukuliwa
hatua za kisheria, ikiwemo mashauri yao kupelekwa
polisi na hivi sasa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia
Rushwa (Takukuru), wanafanya uchunguzi na
hatimaye watuhumiwa hao wafikishwe kwenye
vyombo vya juu vya sheria.
Aidha, maofisa utumishi 233 waliohusika kwenye
malipo ya mishahara hewa mashauri yao,
wamefikishwa kwenye mamlaka husika kwa
uchunguzi, ilhali watatu wamefukuzwa kazi, huku
wizara ikiendelea kufanya uchunguzi kwenye taasisi
75 za umma ili kujiridhisha kuhusu suala la
watumishi hewa.
Kuhusu waajiri 145 ambao hawajawasilisha taarifa
za uhakiki wa watumishi wao, Kairuki alisema zimo
taasisi, wakala, bodi, mabaraza, vyuo, hospitali,
ofisi za Makatibu Tawala wa Mikoa, tume na
mamlaka kadhaa ambazo hazijawasilisha taarifa
zao.
Kwa upande wa mabaraza nchini, Kairuki alisema
mabaraza mbalimbali 10 hayajawasilisha taarifa za
uhakiki wa watumishi na baadhi yao ni kama vile
Baraza la Taifa la Mazingira (NEMC), Baraza la
Elimu ya Ufundi (Nacte), Baraza la Taifa la
Biashara (TNBC), Baraza la Mitihani la Taifa
(NECTA) na Baraza la Michezo la Taifa (BMT).
Aidha, jumla ya vyuo vya umma 25 nchini
havijawasilisha taarifa zao za uhakiki wa watumishi
hewa na baadhi yao ni Dodoma (Udom), Chuo
KIkuu Huria (OUT), Chuo Kikuu Mzumbe, Chuo
Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili
(MUHAS), Chuo cha Diplomasia, Chuo Kikuu cha
Elimu Dar es Salaam (Duce), Chuo cha Usimamizi
wa Fedha (IFM) na Chuo cha Kumbukumbu ya
Mwalimu Nyerere na Chuo Cha Taifa cha
Usafirishaji (NIT).
Upande wa Bodi mbalimbali ambazo hazijawasilisha
taarifa zao jumla yake ni 10 na baadhi ya bodi hizo
ni pamoja na Bodi ya Korosho Tanzania, Bodi ya
Tumbaku, Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu
ya Juu (HESLB) na Bodi ya Utalii na Bodi ya
Maziwa.
Pia zimo hospitali teule za rufaa tatu ambazo ni
Hospitali ya CCBRT, Hospitali ya Rufaa Bugando
na Hospitali ya Rufaa KCMC na kwamba katika
hospitali kama hizo zilizowasilisha taarifa zake,
wamebainika na kuondolewa watumishi hewa 4,000.
Kwenye taasisi za Umma na Wakala ambazo
hazijawasilisha taarifa zao jumla ziko 30 na baadhi
yao ni Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Mfuko
wa Pembejeo za Kilimo, Makumbusho ya Taifa,
Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC), Shirika la
Viwango Tanzania (TBS), Shirika la Madini la Taifa
(Stamico), Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI),
Wakala wa Vitambulisho vya Taifa (NIDA) na
Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC).
Pia zipo Ofisi za Makatibu Tawala wa Mikoa 12
ambazo baadhi yake ni Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa
wa Arusha, Dodoma, Dar es Salam, Mbeya, Pwani
na Kagera; kwa upande wa mamlaka zipo sita
ambazo ni Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA),
Mamlaka ya Maeneo Maalumu ya Uwekezaji kwa
Mauzo ya Nje (EPZA), Mamlaka ya Udhibiti wa
Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) na Mamlaka ya
Ustawishaji Makao Makuu (CDA).
Aidha, zipo tume 10 ambazo hazijawasilisha taarifa
zake na baadhi yake ni Tume ya Pamoja ya Fedha,
Tume ya Atomiki, Tume ya Elimu Taifa, Tume ya
Kudhibiti Dawa za Kulevya, Tume ya Sayansi na
Teknolojia Tanzania na Tume ya Vyuo Vikuu
Tanzania (TCU).
Pia zipo Mamlaka za Serikali za Mitaa 38 zikiwemo
Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Manispaa ya Iringa,
Nyamagana, Halmashauri ya Mji, Kasulu,
Halmashauri ya Wilaya ya Dodoma na Halmashauri
ya Wilaya ya Misenyi.
Wednesday, 17 August 2016
WAZIRI WA ELIMU ATOA WIKI MOJA VYUO VIREJESHE FEDHA
Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania, Prof. Joyce Ndalichako ametoa siku saba kwa vyuo vikuu vilivyopokea fedha za wanafunzi ambao hawapo vyuoni kwa mwaka wa 2015/16 kuzirejesha wizarani mara moja.
Taarifa hiyo ameitoa jana jijini Dar es Salaam mbele ya maafisa kutoka wizarani mwake,pamoja na kaimu mkurugenzi mtendaji wa bodi ya mikopo.
Thursday, 11 August 2016
FAIDA 13 ZA KULA PILIPILI
1.Kutibu kidonda-Hii inaweza kuwa ni ajabu kwa walio wengi lakini ni tiba liyothibitishwa na imekuwa ikitumika miaka kadhaa iliyopita katika nchi mbalimbali.Sio tu kuzuia kutokwa na damu katika kidonda cha kujikata kama ilivyozoea kutumiwa na wengi huko majumbani kwa miaka mingi bali pia huzuia fangasi na bakteria kuingia katika uwazi wa kidonda hicho hutumika pia kuondoa sumu mwilini
2.Hufanya mwili kuweza kutumia vyema virutubisho vipatikanavyo kutokana na chakula
3.Husaidia uyeyushaji wa mafuta mwilini/Kuchoma mafuta
4.Pilipili ina antioxidants muhimu kama beta carotene,ina wingi wa vitamini A,C na K hebu tuziangalie vitamini hizo:
(i)Vitamini A husaidia kuweka sawa kinga ya mwili pia hutukinga na kansa na magonjwa ya moyo
(ii) Kazi ya vitamini C-ni kuzuia Stroke,magonjwa ya moyo,macho na kansa mbalimbali.Miili ya binadamu haiwezi kujitengenezea vitamini C,hivyo basi tunaweza kupata vitamini C kupitia chakula.
(iii) Vitamini K-Husaidia katika ukuwaji wa mifupa,pia ni muhimu katika mzunguko wa damu.Pilipili zote huwa na Capsaicin ambayo kazi yake ni kupunguza maumivu,kuzuia kansa na magonjwa ya moyo.
5.Inasaidia sana kusawazisha sukari kwenye damu
6.Huwasaidia watu wanene(over weight) au wanaougua ugonjwa wa kisukari.Hii ni kwa mujibu wa watafiti katika chuo kikuu cha Tasmania uliochapishwa katika American Joarnal of Clinical Neutition mwezi julai 2006.
7.Inasaidia kwa kiasi kikubwa kudhibiti kwa kiasi kikubwa INSULIN kwa 60% baada ya kula chakula
8.Husaidia kupunguza maumivu na uvimbe kwenye tezi na vilevile huwasaidia wagonjwa wa RHEMATOID na ARTHRITIS kupata nafuu
9.Husaidia kuondoa mkusanyiko wa damu sehemu moja mwilini
10.Husaidia kufungua kwa haraka na kwa ufanisi pua zilizoziba kwa mafua na kukufanya upumue kwa urahisi.
11.Husaidia kupunguza uwezekano wa kupatwa na saratani ya utumbo.
12.Husaidia kuongezeka kwa kiwango cha METABOLIC kwa 23% ndani ya masaa matatu baada ya kuitumia. Hii pia husaidia kuchoma mafuta katika mwili.
13.Husaidia kupunguza cholestro na kupunguza kiasi cha fibrin katika damu.