Almasi Mswahili

Thursday, 11 August 2016

FAIDA 13 ZA KULA PILIPILI

1.Kutibu kidonda-Hii inaweza kuwa ni ajabu kwa walio wengi lakini ni tiba liyothibitishwa na imekuwa ikitumika miaka kadhaa iliyopita katika nchi mbalimbali.Sio tu kuzuia kutokwa na damu katika kidonda cha kujikata kama ilivyozoea kutumiwa na wengi huko majumbani kwa miaka mingi bali pia huzuia fangasi na bakteria kuingia katika uwazi wa kidonda hicho hutumika pia kuondoa sumu mwilini

2.Hufanya mwili kuweza kutumia vyema virutubisho vipatikanavyo kutokana na chakula

3.Husaidia uyeyushaji wa mafuta mwilini/Kuchoma mafuta

4.Pilipili ina antioxidants muhimu kama beta carotene,ina wingi wa vitamini A,C na K hebu tuziangalie vitamini hizo:
(i)Vitamini A husaidia kuweka sawa kinga ya mwili pia hutukinga na kansa na magonjwa ya moyo
(ii) Kazi ya vitamini C-ni kuzuia Stroke,magonjwa ya moyo,macho na kansa mbalimbali.Miili ya binadamu haiwezi kujitengenezea vitamini C,hivyo basi tunaweza kupata vitamini C kupitia chakula.
(iii) Vitamini K-Husaidia katika ukuwaji wa mifupa,pia ni muhimu katika mzunguko wa damu.Pilipili zote huwa na Capsaicin ambayo kazi yake ni kupunguza maumivu,kuzuia kansa na magonjwa ya moyo.

5.Inasaidia sana kusawazisha sukari kwenye damu

6.Huwasaidia watu wanene(over weight) au wanaougua ugonjwa wa kisukari.Hii ni kwa mujibu wa watafiti katika chuo kikuu cha Tasmania uliochapishwa katika American Joarnal of Clinical Neutition mwezi julai 2006.

7.Inasaidia kwa kiasi kikubwa kudhibiti kwa kiasi kikubwa INSULIN kwa 60% baada ya kula chakula

8.Husaidia kupunguza maumivu na uvimbe kwenye tezi na vilevile huwasaidia wagonjwa wa RHEMATOID na ARTHRITIS kupata nafuu

9.Husaidia kuondoa mkusanyiko wa damu sehemu moja mwilini

10.Husaidia kufungua kwa haraka na kwa ufanisi pua zilizoziba kwa mafua na kukufanya upumue kwa urahisi.

11.Husaidia kupunguza uwezekano wa kupatwa na saratani ya utumbo.

12.Husaidia kuongezeka kwa kiwango cha METABOLIC kwa 23% ndani ya masaa matatu baada ya kuitumia. Hii pia husaidia kuchoma mafuta katika mwili.

13.Husaidia kupunguza cholestro na kupunguza kiasi cha fibrin katika damu.

No comments:

Post a Comment