Almasi Mswahili

Tuesday, 13 September 2016

CWT:MADENI YA WALIMU HAYAJAKWISHA

Hayo yamesemwa na rais wa chama cha walimu Tanzania Bw. Gracian Mukoba kufuatia kauli iliyotolewa na serikali mwishoni mwa wiki iliyopita kupitia waziri wa mwenye dhamana Prof. Joyce Ndalichako kuwa serikaili tayari imekamiliza kulipa madeni yote ya walimu. Akizungumza na waandishi wa habari jana rais wa chama cha walimu amesema kuwa taarifa hizo sio sahihi kwa sababu bado kuna walimu kutoka halmashauri mbalimbali bado wanaidai serikali madeni mbalimbali yakiwemo yasiyokuwa ya mishahara,aliongeza kuwa hakufuraishwa na hatua hiyo ya serikali kutoa taarifa hizo kwani zinaweza kuwafanya walimu wafikiri kuwa serikali inataka kuwadhulumu pia ameitaka serikali kupitia tena madeni ya walimu ili kuondoa sintofahamu ambayo inaweza kujitokeza katika siku zijazo.

No comments:

Post a Comment