Almasi Mswahili

Wednesday, 12 October 2016

SAKATA LA MBEYA DAY RC KAYAONGEA HAYA

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makala
amesema kuwa wanafunzi wa ualimu na walimu
waliohusika na tukio la kumpiga mwanafunzi
katika Shule ya Sekondari ya Kutwa Mbeya tayari
wanaendelea kuhojiwa na Jeshi la Polisi kufuatia
tukio hilo.
Licha ya kuwa tukio lile halikuwa adhabu sahihi
kwa mwanafunzi, Mkuu wa Mkoa amewataka
wazazi kujijengea tabia ya kuwafuatilia watoto wao
kwani ameleeza kuwa nidhamu ya wanafunzi wa
shule hiyo ni mbovu sana hasa kwa wanafunzi wa
kidato cha tatu na cha nne.
Mkuu wa mkoa ameeleza kuwa, kuna wakati
darasa lenye wanafunzi 50, mwalimu anafundisha
wanafunzi 10 pekee wengine wakiwa hawamo
darasani na mara kadhaa wanapishana na
mwalimu wakati wanaingia wao wanatoka.
Wanafunzi wengine wamediriki hata kukunjiana
ngumi na walimu, hivyo baadhi ya walimu ili
kuepusha shari wamewaacha wafanye waoonavyo
vyema.
Mkuu wa mkoa amesema kuwa wataendelea
kufanya uchunguzi kuwabaini wanafunzi wakarofi
zaidi na adhabu stakihi zitachukua hatua mara
moja ili kuweza kurejesha nidhamu katika shule
mkoani humo.
***********************************
Mswahili

No comments:

Post a Comment