Bodi ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu
(HESLB) imetuliza hasira za wanafunzi wa vyuo
vikuu kwa kurejesha posho ya chakula na malazi
ya Sh8,500 kwa kila mmoja na kwamba tofauti
baina yao itakuwa viwango vya ada.
Ufafanuzi huu uliotolewa jana usiku na Waziri wa
Elimu, Sayansi , Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi
Profesa Joyce Ndalichako wakati akizungumza
katika mahojiano maalimu na kituo cha runinga
cha Taifa -TBC utakuwa faraja kwa wanafunzi
ambao chini ya Serikali ya Wanafunzi wa Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam (Daruso) walipanga
kushinikiza walipwe posho ya Sh8,500 kwa siku
kama ilivyokuwa awali.
Hatua ya wanafunzi kujenga umoja ili kushinikiza
haki katika posho ilitokana na baadhi yao
kuingiziwa kati ya Sh40,000 na 70,000 badala ya
Sh 510,000, hali ambayo ilizua sintofahamu.
Ndalichako alisema tofauti ya malipo itakuwa
katika ada na siyo posho, “Vigezo vya mikopo
vimebadilika, kila mwanafunzi atapata fedha tofauti
lakini tumefanya marekebisho kwenye posho ya
chakula ambayo kila mwanafunzi atalipwa Sh8,500
kama awali.”
Kwa mujibu wa utaratibu wa Bodi hiyo, malipo
hayo ya chakula na malazi hutolewa kila baada ya
miezi miwili.
Mapema jana, Daruso iliwataka wanafunzi wa chuo
hicho kutotia saini fomu za fedha za mikopo yao
mpaka itakapowapa ruhusa ya kufanya hivyo.
Rais wa Daruso, Erasmi Leon alisema hayo jana
wakati akizungumza na wanafunzi wenzake kuhusu
kusudio la kwenda HESLB kwa ajili ya kutafuta
haki yao ya msingi.
“Ninachowasihi tuwe pamoja. Tuwe wamoja na
twende pamoja. Tutakwenda wawakilishi kutafuta
nafasi kwa amani waweze kusikia tuna hoja gani
lakini tukinyimwa hii nafasi tutaenda kuitafuta
tukiwa wengi,” alisema na kuongeza:
“Tuwe watulivu kwa sasa tutakapowahitaji muda
na wakati wowote kwa lolote tushirikiane ili twende
pamoja tumalize pamoja tuhakikishe tunapata
Sh8,500 kwa kila mwanafunzi kwa chakula na
malazi,” alisema.
Kuhusu suala hilo, uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar
es Salaam (UDSM) ulisema wajibu wake ni
kupokea na kusambaza majina na taarifa kutoka
Bodi kwa wanafunzi.
Akitoa ufafanuzi kwa wanafunzi waliofika ofisini
kwake kujua hatima yao na waliopata mikopo
kuchukua fomu za kutia saini, Ofisa Mikopo wa
UDSM, Lugano Mwakyusa alisema wenye jukumu
la kujua walio na sifa ya kupata mikopo ni Bodi ya
Mikopo.
“Tunaendelea kupokea majina kutoka bodi. Tayari
hapa kuna majina 949 yameshatoka, wengine tuzidi
kusubiri na wale mwaka wa pili na tatu ambao
walikuwa na mitihani ya marudio taarifa zao
zitapelekwa bodi,” Mwakyusa aliwaambia
wanafunzi waliokuwa wamejaa ofisini kwake.
Kulikuwa na hali ya sintofahamu chuoni hapo jana
baada ya wanafunzi wengi wa mwaka wa kwanza
kuonekana wakiwa wameshika bahasha za kaki
zilizokuwa na fomu za usajili wanazotakiwa kujaza
huku wakihangaika kutokana na kutojua kiasi cha
mkopo.
Juzi, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, AbdulRazaq
Badru alieleza kwamba ingawa wanafunzi 88,000
waliomba mikopo kutoka HESLB, uwezo wa bodi
hiyo ni kutoa kwa wanafunzi 21,500 pekee sawa
na asilimia 24 na waliokuwa wameshapatiwa
walikuwa 11,000 sawa na asilimia 12.
Takwimu hizi zinaonyesha zaidi ya robo tatu ya
wanafunzi wanaohitaji mikopo watakosa kutokana
na uwezo mdogo wa kifedha.
Welcome to our blog,this blog is deals with the all news about education and it allow teachers and other education dealers to discuss different things.
Thursday, 20 October 2016
MIKOPO KWA WANAOSOMA VYUO VIKUU BADO NI KIZUNGUMKUTI.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment