Hayo yamesemwa na rais wa chama cha walimu Tanzania Bw. Gracian Mukoba kufuatia kauli iliyotolewa na serikali mwishoni mwa wiki iliyopita kupitia waziri wa mwenye dhamana Prof. Joyce Ndalichako kuwa serikaili tayari imekamiliza kulipa madeni yote ya walimu. Akizungumza na waandishi wa habari jana rais wa chama cha walimu amesema kuwa taarifa hizo sio sahihi kwa sababu bado kuna walimu kutoka halmashauri mbalimbali bado wanaidai serikali madeni mbalimbali yakiwemo yasiyokuwa ya mishahara,aliongeza kuwa hakufuraishwa na hatua hiyo ya serikali kutoa taarifa hizo kwani zinaweza kuwafanya walimu wafikiri kuwa serikali inataka kuwadhulumu pia ameitaka serikali kupitia tena madeni ya walimu ili kuondoa sintofahamu ambayo inaweza kujitokeza katika siku zijazo.
Welcome to our blog,this blog is deals with the all news about education and it allow teachers and other education dealers to discuss different things.
Tuesday, 13 September 2016
WANAFUNZI WAWATANDIKA FIMBO WALIMU WAO
Wawanafunzi wa Kidato cha Sita Shule ya
Sekondari Usevya wilayani Mlele Mkoa wa Katavi,
wanadaiwa kuwashambulia kwa kuwacharaza viboko
walimu wao wawili miongoni mwao akiwemo Makamu
Mkuu wa Shule hiyo, Makonda Ng’oka
“Membele'‘ (34) ambaye ameng’olewa meno
matano kwa kipigo hicho.
Walimu hao wawili wamedai kuwa hawako tayari
kuendelea kufundisha katika shule hiyo huku
wakisisitiza kuwa ni fedheha kwao kucharazwa
viboko na wanafunzi wao wenyewe ambapo Mwalimu
Gabriel Kambona aliachwa na ngeu kichwani.
Mei mwaka huu, Ng’oka “Membele” alifikishwa
katika Mahakama ya Mkoa wa Katavi kwa tuhuma
za kumlawiti mwanafunzi wake akidaiwa kutenda
kosa hilo kati ya Novemba 2015 na Aprili mwaka
huu.
Ilisemekana kukamatwa na kufikishwa mahakamani
kwa Makamu Mkuu huyo wa shule hiyo kulifuatia
wanafunzi wa kiume wanaosoma Kidato cha Tano
sasa wako Kidato cha Sita katika shule hiyo
kumkataa na kutishia kuandamana kupinga vitendo
vyake vya kuwalawiti wanafunzi wake.
Wanafunzi hao walidai kuwa mwalimu huyo
amekuwa akiwalawiti baadhi yao ikiwa ni adhabu
mbadala wanapobainika kufanya makosa shuleni
hapo.
Hata hivyo, baada ya kutopatikana ushahidi wa
kumtia hatiani Ng’oka, Julai 27, mwaka huu
Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Wilaya ya Mpanda
ilimwachia huru.
Mwalimu Ng’oka aliripoti kwenye kituo chake cha
kazi shuleni Usevya Agosti Mosi mwaka huu ambako
kurejea kwake shuleni hapo kunadaiwa kuamsha
hasira kwa baadhi ya wanafunzi wa Kidato cha Sita
wakidai hawapo tayari kumwona mwalimu huyo na
familia yake shuleni hapo.
Akizungumza na wanahabari jana mjini hapa,
Ng’oka alidai kuwa hayuko tayari kuendelea
kufundisha kwenye shule hiyo akihofia usalama
wake na kutokana na kipigo alichokipata cha
kushambuliwa na baadhi ya wanafunzi wake wa
kidato cha tano na cha sita wakati akiwa nyumbani
kwake na familia yake.
Akisimulia mkasa huo, alisema Agosti 12, mwaka
huu usiku alikuwa nyumbani kwake shuleni hapo
pamoja na familia yake pamoja na mwalimu
mwenzake, Gabriel Kambona aliyekuwa
amemtembelea.
“Ghafla, saa mbili usiku nikiwa maliwatoni nikioga
lilitokea kundi la wanafunzi wa kidato cha tano na
sita wakiwa na silaha za jadi kama vile fimbo,
marungu, mawe na matofali na kuanza
kuishambulia familia yangu pamoja na mwalimu
Kambona,” alieleza na kuongeza kuwa alilazimika
‘kuchomoka’ bafuni baada ya kusikia mayowe
yaliyokuwa yakipigwa na familia yake wakiomba
msaada. Alipofika sebuleni alishuhudia wanafunzi
hao wakiishambulia familia yake kwa kuwacharaza
viboko.
“Ndipo walinigeukia na kuanza kunishambulia kwa
kunipiga kwa marungu na fimbo hadi nikapoteza
fahamu nilizinduka nikiwa nimelazwa kwenye Kituo
cha Afya Usevya na kubaini kuwa nimepoteza meno
yangu matano huku nikiwa nimejeruhiwa vibaya
kichwani. Baadaye nilihamishiwa katika Hospitali
ya Wilaya ya Mpanda ambako nililazwa wiki moja na
nusu kwa matibabu na sasa nimepewa rufaa niende
Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar kwa
matibabu zaidi,” alieleza.
Alidai kuwa uhasama baina yake na wanafunzi hao
umedumu kwa muda mrefu, lakini anashangaa
uongozi wa Halmashauri ya Mpimbwe na Wilaya ya
Mlele umeshindwa kumpangia kituo kingine cha
kazi na kuchukua hatua yoyote kwa wanafunzi hao
licha ya kupeleka majina yao kwa kuwa
anawafahamu wote waliohusika.
Mwalimu Kambona alidai kuwa hayuko tayari
kuendelea kufundisha kwenye shule hiyo kwamba
kitendo cha kupigwa na wanafunzi wake
kimemfedhehesha.
Kwa mujibu wa mwalimu huyo, walimu wa shule hiyo
waliketi baada ya kutokea kwa tukio hilo, na
walifikia maamuzi kuwa wanafunzi wote
waliobainika kushiriki kuwashambulia walimu wao
wasimamishwe shule akidai kuwa uongozi wa
Halmashauri ya Mpimbwe na Wilaya ya Mlele
ulipinga.
“Nimeandika barua ya kuomba uhamisho kwani nia
aibu kwangu kuendelea kufundisha wanafunzi
ambao wamenishambulia na kunitoa ngeo kichwani
….. siku hiyo ya tukio niliibiwa simu mbili za
kiganjani lakini jana nimefanikiwa kuikamata simu
moja kwa mwanafunzi wa kidato cha tano
anayeitwa , Alex Maiko Makona na tayari
amemfikisha katika Kituo cha Polisi cha Usevya,”
alidai.
Mwenyekiti wa Chama cha Walimu (CWT) Mkoa wa
Katavi, Gregori Mshota alisema tayari chama
chake kimeanza kuwasiliana na uongozi wa
Halmashauri ya Mpimbwe na uongozi wa Wilaya ya
Mlele ili kuhakikisha mwalimu huyo anakuwa
salama.
Ofisa Elimu wa Mkoa wa Katavi, Ernest Hinju
alidai kuwa suala hilo lipo ofisini kwake na
wameanza kulitafutia ufumbuzi. “Jambo hili
linahitaji ushirikishwaji wa vyombo mbalimbali
ikiwemo Bodi ya Shule ya Sekondari ya Usevya,”
alieleza.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipokuwa katika
ziara mkoani Katavi mwezi uliopita, mke wa
mwalimu Ng’oka alitinga kwenye mkutano wa
hadhara uliofanyika kijijini Maji Moto akiwa na
bango lenye malalamiko ya kutishiwa usalama wa
maisha wa familia yake, na Waziri Mkuu alimwagiza
Kamanda wa Polisi wa Mkoa kushughulikia
malalamiko hayo.
CHAGUZI KWA WALIOOMBA VYUO VIKUU
Tume ya vyuo vikuu imetoa orodha ya majina ya waliochaguliwa katika vyuo mbalimbali nchini kuangalia bofya hapa👇 http://cas.tcu.go.tz/cas_core/index
AJIRA MPYA ZANUKIA
Serikali imeanza kupanga walimu wa sayansi moja
kwa moja katika shule badala ya Halmashauri kama
ilivyokuwa awali ili kuleta uwiano sawa wa walimu
katika shule mbalimbali nchini.
Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Rais (TAMISEMI) Suleman Jaffo alipokuwa
akijibu swali la Mbunge wa Muleba Prof. Anna
Tibaijuka lililohusu mkakati wa Serikali katika
kukabiliana na tatizo la upungufu wa walimu.
Naibu Waziri Jaffo amesema kuwa Serikali
imeandaa mkakati wa kuwaajiri wahitimu wa
shahada za sayansi ambazo siyo za ualimu baada ya
kuwapa mafunzo ya muda mfupi kuhusu mbinu za
ufundishaji na maadili ya ualimu ili kukabiliana na
changamoto ya walimu wa sayansi nchini.
Naibu Waziri Jaffo amesema kuwa tayari kibali
kimeombwa katika Ofisi ya Rais Utumishi kwa ajili
ya utekelezaji huo, ambapo Serikali imepanga
kuajiri walimu wastaafu wenye uwezo wa
kufundisha waliokuwa wanafundisha masomo ya
sayansi kwa mkataba ili kupunguza pengo lililopo.
Aidha, Naibu Waziri Jaffo amebainisha kuwa
Serikali inafanya tathimini ya mahitaji ya walimu
wa masomo ya sanaa kwa kila Halmashauri ili
kubaini maeneo yenye ziada na yenye upungufu ili
kusawazisha.
“Mpango wa Serikali uliopo ni kuwahamasisha
walimu wa ziada wa masomo ya sanaa kwenda
kufundisha katika shule za msingi ndani ya
Halmashauri husika, ambapo kabla ya kuanza
utekelezaji wa mabadiliko haya Serikali itatoa
waraka maalumu kwenda katika Halmashauri zote
nchini ” amefafanua Naibu Waziri huyo.
Akizungumzia kuhusu utaratibu wa mafunzo ya
walimu Mhe. Jaffo amesema kuwa Halmashauri
moja haiwezi kuwa na mfumo wa peke yake wa
kuandaa walimu hali ambayo iltakuwa ni vigumu
kuthibiti ubora wa mafunzo hayo kwa walimu.
Hata hivyo amesema kuwa Serikali itaendelea
kuongeza udahili wa walimu wa sayansi katika vyuo
vya ualimu kadri watakavyojitokeza ili kukidhi
mahitaji yaliyopo
Saturday, 10 September 2016
WAZIRI:TUMESHAMALIZANA NA WALIMU
WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia
na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce
Ndalichako amesema hadi sasa wizara
hiyo haina deni inayodaiwa na walimu
nchini na kwamba madeni yaliyokuwepo
ya Sh bilioni 22 yalishalipwa.
Profesa Ndalichako alisema hayo juzi
jioni wakati akizungumza kwenye
kipindi cha Tunatekeleza
kinachorushwa hewani moja kwa moja
na Kituo cha Televisheni cha Shirika
la Utangazaji Tanzania (TBC1).
Akizungumzia madeni ya walimu,
alisema serikali inawajali walimu
nchini na zipo jitihada mbalimbali
zimekuwa zikifanywa kuhakikisha madai
yao yanahakikiwa na kulipwa ili
kuepuka malimbikizo.
Alisema madeni ya walimu yako ya
aina mbili; moja ni madeni ya
mishahara ambayo wao wizara
hawayashughulikii bali yapo chini ya
Ofisi ya Rais, Utumishi na kwamba
madai aina ya pili ni yale yasiyo na
mshahara kama vile likizo, matibabu
na mengineyo, ambayo yako chini ya
wizara yake na hadi sasa wameshalipa
Sh bilioni 22 na hakuna madeni
mengine kutoka kwa walimu na
kuwataka walimu nchini kama wana
madeni mapya kuanzia sasa
wayawasilishe wizarani kwa ajili ya
kuhakikiwa na kulipwa.
“Wizara tunatambua mchango wa walimu
na umuhimu wao kwa upande wetu,
hatuna madai yoyote ya walimu yale
yanayotuhusu, kwa sababu huwa tuna
utaratibu wa kulipa kadri
tunavyoyapata na kama yapo kwa sasa
wayalete, fedha za kulipa zipo,”
alisema Profesa Ndalichako.
Akizungumzia suala la watumishi
hewa, Profesa Ndalichako alisema ni
vyema walioguswa katika uhakiki huo
unaoendelea kufanywa na timu ya
watendaji kutoka taasisi mbalimbali,
wakiwemo wakurugenzi, wakajiondoa
wenyewe kwenye ajira kwa sababu
mashtaka yanawangoja.
Kuhusu uhakiki wa wanafunzi wa elimu
ya juu, Profesa Ndalichako alisema
hadi sasa wamekamilisha uhakiki wa
vyuo 31 kati ya vyuo 80 vilivyopo
nchini na wameshabaini wanafunzi hewa
2,921 ambao hawakujitokeza wakati wa
uhakiki, licha ya matangazo na
msisitizo kutolewa.
Profesa Ndalichako alisema wakati
kazi ya uhakiki ilipoanza, walitoa
matangazo katika vyuo vyote na pia
vyuo navyo vilitoa matangazo kwenye
mbao za matangazo vyuoni na pia
kupitia vyombo vya habari na pia
kupitia serikali ya wanafunzi katika
vyuo husika, lakini idadi hiyo
haikujitokeza kuhakikiwa.
Alisema kwa wale wachache waliopuuza
kuhakikiwa hata kama wako mwaka wa
mwisho wa masomo, bado watatambulika
kama wanafunzi hewa hadi pale
watakapohakikiwa na hiyo itawagharimu
kulipa gharama za kufanyiwa uhakiki
huo.
Akizungumzia changamoto za wanafunzi
kutojua kusoma na kuandika, Profesa
Ndalichako alisema serikali imekuwa
imetoa mafunzo kwa walimu
wanaofundisha darasa la kwanza na la
pili na kwamba kadri muda
unavyosonga ndivyo tatizo
linavyoondoka.
Kuhusu utaratibu wa utoaji mikopo
kwa elimu ya juu, Profesa Ndalichako
alisema changamoto zipo kutokana na
mfumo uliokuwa ukitumika, lakini
hatua zimeshaanza kuchukuliwa ili
kuuboresha ili kuhifadhi kumbukumbu
za wanufaika ili iwe rahisi kuzidai.
Aidha, alisisitiza wanafunzi
waliomaliza shahada zao katika vyuo
mbalimbali nchini na ikagundulika
kuwa walizipata kwa njia ya rushwa,
ikibainika watanyang’anywa.
Chanzo: Habari Leo.
Tuesday, 6 September 2016
ONYO KWA WASIMAMIZI MTIHANI WA DARASA LA SABA
Na Almasi Mswahili
Ikiwa yamesalia masaa kadhaa kabla ya kuanza kwa mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi hapo kesho na kesho kutwa (Jumatano tarehe 7/9/2016 na Al-hamis tarehe 8/9/2016)
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya
Ileje Haji Mnasi, amewaasa wasimamizi wa mitihani
ya kumaliza elimu ya msingi kutofanya kazi kwa
mazoea ili kutoruhusu mianya itakayowafanya
wanafunzi wasiokuwa na uelewa kufaulu mitihani
hiyo.
Alisema kumekuwa na baadhi ya wanafunzi
wasiojua kusoma na kuandika wanafaulu mithani
hiyo kitendo kinachotia mashaka kwa wasimamizi
hao kushindwa kunyakazi waliyopewa kwa makini.
Mnasi aliyasema hayo jana, wakati akitoa semina
ya mafunzo kwa wasimamizi wa halmashauri ya
wilaya ya Ileje ambapo alisema usimamizi hafifu wa
mitihani umesababisha kuwepo kwa watumishi
wasiokuwa na uwezo kitaaluma.
Aidha kabla ya uteuzi wa Rais wa jamhuri ya
muungazo wa tanzania Dr John Pombe Magufuli
mkurugenzi huyo ambaye kitaaluma ni mwalimu
alikuwa afisa elimu shule ya msingi manispaa ya
iringa alisema iwapo ikibainika kufaulu kwa
wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika mtuhumiwa
wa kwanza kwenye uzembe huo atakuwa msimamizi
wa mitihani na hatua kali zitachukuliwa zidi yake.
“Nawatahadharisha kwamba mnaweza mkarubuniwa
kuwawezesha wanafunzi wasiokuwa na sifa wafaulu
mitihani hiyo,kufanya hivyo ni kukiuka kanuni za
usimamizi na uendeshaji wa mtihani na kuwaambia
hayupo tayari kutumbuliwa na rais kwasababu za
wasimamizi”alisisitiza Mnasi.
Hata hivyo Mnasi aliwataka wasimamizi hao kuwa
makini katika kufanyakazi hiyo na kama kuna
jambo lolote ambalo hawajalielewa kuhusu kazi hiyo
ni vyema wakauliza ili kupewa majibu.
“hakikisheni kuwa taratibu zote za mitihani
zinazingatiwa ipasavyo na kuwataka wasimamizi
wote kufanya kazi yao kwa umakini na uadilifu wa
hali ya juu.“Nawaasa wasimamizi wa mitihani
kujiepusha na vitendo vya udanganyifu kwani
serikali itachukua hatua kali kwa yeyote
atakayebainika kukiuka taratibu za mitihani,”
alisema Mnasi.
Mnasi alibainisha kuwa, serikali imezingatia uwezo
wa kitaaluma, uadilifu na uaminifu hivyo
wasimamizi hao kupewa jukumu la kusimamia
mitihani hiyo muhimu ya kitaifa.
Aliongeza kuwa mitihani hiyo ni muhimu ili
kuliwezesha taifa kupima kiwango cha elimu
kilichpo nchini na kuwapata wasomi wa kiwango cha
juu.
Nao wasimamizi wa mitihani hiyo wamemuahidi
mkurugenzi huyo kuwa watasimamia mitihani hiyo
kwa kufuata sheria na kanuni za usimamizi wa
mitihani walizopewa.
Saturday, 3 September 2016
WIZARA YA ELIMU YATAKIWA KUONGEZA WATAALAMU WA AFYA
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameitaka Wizara ya
Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi iweke mpango
maalumu wa kuongeza wataalamu zaidi katika
sekta ya afya ndani ya nchi ili kuipunguzia Serikali
gharama za kusomesha wataalam hao nje ya nchi.
Ametoa agizo hilo Ijumaa, Septemba 2, 2016
wakati alipokagua maendeleo ya mradi wa ujenzi
wa Kampasi ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Afya na
Sayansi ya Tiba Muhimbili (MUHAS) na Ujenzi wa
Kituo cha Tiba cha Kimataifa cha Muhimbili katika
eneo la Mloganzila.
Amesema Serikali zilizotangulia zimefanya kazi
kubwa na nchi imefikia hatua nzuri ya kuongeza
wataalam ndani ya nchi ambao watakwenda
kutatua changamoto ya upungufu wa madaktari
bingwa kwenye hospitali za mikoa na wilaya.
Waziri Mkuu amesema ujenzi wa kituo hicho cha
tiba cha kimataifa pia utawapunguzia wananchi
adha ya kutafuta fedha za kwenda kupata
matibabu nje ya nchi. Tayari upasuaji mkubwa wa
magonjwa ya moyo umeanza kufanyika nchini.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amemuagiza
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Bw. Humphrey
Polepole awasake watu wote waliohusika na wizi wa
lita 1,000 za mafuta ya kuendeshea mitambo
katika karakana ya mkandarasi anayejenga
Kampasi hiyo.
“Wafanyakazi waache wizi. Lita 1,000 zinaondokaje
katika karakana ya mkandarasi? Hii kampuni
inayolinda kama imeshindwa kazi iondolewe na
Mkuu wa wilaya usimhurumie mwizi,” amesisitiza.
Kwa upande wake Waziri wa Elimu, Sayansi na
Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako amesema
kukamilika kwa kampasi ya Mloganzila kutasaidia
upatikanaji wa madaktari bingwa wengi nchini
ambao watapunguza gharama za kupeleka
wagonjwa kwenda kutibiwa nje ya nchi.
Awali, Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Ephata
Kaaya alisema kukamilika kwa hospitali pamoja na
kampasi yote ya chuo kutawezesha kupunguza kwa
kiasi kikubwa uhaba wa wataalamu wa afya nchini.
Amesema hospitali hiyo itatumika kutoa huduma za
afya za kitaalam zaidi kwa magonjwa mbalimbali,
hivyo kupunguza idadi ya wagonjwa wanaopelekwa
nje ya nchi kwa matibabu. Pia itapunguza
msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Taifa
ya Muhimbili.
Ujenzi wa mradi huo umegharimu Dola za
Kimarekani milioni 61, ambapo Serikali imetoa Dola
milioni 18 na Serikali ya Korea imetoa mkopo wa
Dola milioni 43. Kukamilika kwa ujenzi wa kampasi
hiyo ya Mloganzila kutawezesha chuo kuongeza
idadi ya udahili wa wanafunzi wa fani ya afya
kutoka 4,010 hadi 15,000.
Prof. Kaaya amesema mkataba wa awamu ya
kwanza ya ujenzi wa mradi huo ulisainiwa tarehe
12, Desemba, 2014 na ujenzi ulianza mwezi Julai,
2015 na unatarajiwa kukamilika Oktoba, 2016.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
Friday, 2 September 2016
TCU YATANGAZA UDAHILI AWAMU YA PILI
Tunapenda kuutangazia Umma kuwa tulifunga
mfumo wa pamoja wa udahili tarehe 31/08/2016
saa sita usiku ili kuchakata maombi ya waombaji
waliofanikiwa kuomba udahili kwa mwaka wa
masomo 2016/2017.
Hata hivyo kutokana na wengine kushindwa
kufanikiwa kutokana na sababu mbali mbali, Tume
inatangaza kuwa itafungua maombi kwa awamu ya
pili kuanzia tarehe 12 hadi 23 Septemba 2016 ili
kuruhusu makundi yafuatayo kuomba udahili.
1. Waombaji watakaokuwa wamekosa nafasi
kwenye awamu ya kwanza
2. Waombaji wa kidato cha Sita walioshindwa
kuomba katika awamu ya kwanza
3. Waombaji wenye vigezo vya Stashahada ambao
walishindwa kuomba kutokana na matokeo yao
kuchelewa kufika NACTE kwa wakati,
4. Waombaji ambao wamemaliza mitihani ya
“Cambridge” mwaka 2016 na matokeo yao
yameshatoka,
5. Waombaji waliofaulu mitihani ya RPL,
6. Waliokuwa wanafunzi wa vyuo vikuu watakao
kuwa na uthibitisho toka vyuo vyao vya awali.
Baada ya hapo Tume haitaruhusu tena maombi ili
kuruhusu taratibu zingine za kiudahili kuendelea
kwa ngazi ya Bodi ya Mikopo na vyuoni.
Asanteni
Imetolewa na
Prof. Eleuther Mwageni
Kaimu Katibu Mtendaji
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania
02 Septemba 2016